DAMIJA MK MAKENE MICHUZI MWANDANI NDESANJO CHARAHANI AISHA ABDI MAVAZI SHAMIM MAGGID WATANZANIA Jumuia ya Wanablogu wa Tanzania
UNO AU EAC TANZANIA EU NASA REUTERS IPP Muungano wa Vijana Duniani dhini ya UKIMWI TIG IPP
NITUMIE BARUA PEPE

Yaliyojiri Juma Hili!
Wednesday, May 10, 2006
Habari za jioni wanablogu wote wa kiswahili na hata wa lugha nyingine mbalimbali duniani.

Kwanza, nachukua fursa hii adhimu kuwa shukuru wote mliotembelea blogu yangu, wale wote mlionipa pole kutokana na masahibu yaliyonikuta, basi nawashukuru sana sana. Naamini nitapona sawa sawia. Kwa taarifa tu ni kwamba, sasa hivi naendelea vizuri, jicho langu limepunguza maumivu kwa kiasi kikubwa sana, na pia bado nazidi kurudisha uoni.

Leo hii pia nina furaha kubwa sana kuwatambulisha wanablogu wawili wapya kabisa katika ulimwengu wa blogu, lakini pia ni wanaharakati madhubuti wa masuala ya haki za binadamu, haki za watu wenye ulemavu, maendeleo na mambo kadhaa chanya kwetu.

Mmoja kati ya hao wanablogu wapya ni ndugu Mkatambo, yeye ni Afisa Sheria Mkuu hapa Kituo cha msaada wa sheria Magomeni.

Mwingine ni Mtanganyika, huyu mheshimiwa naye mambo yake mjionee tu wenyewe.

Kwa kuwa bado sijawa na utaalam wa kuingiza viunga na pia kuwatangaza hawa jamaa katika blogu yangu, naamini wanablogu wenzangu wenye utaalamu huo mtalibeba jukumu hilo kwa utayari na ukamilifu wake. Hata hivyo, bado ninajitahidi kwa kasi ya ajabu katika kuupitia mwongozo wa wanablogu na miongozo mingine, basi si haba labda siku si chache na mimi nitakuwa mbali katika kujitangaza na kuwatangaza wenzangu.

Kwa J'tano ya leo, yaliyojiri ni hayo, wassalaam nawatakia juma jema.

Karibuni wanaharakati
Muandishi: Kaka Poli Saa: 7:43 pm | Permalink |


0 Comments:


eXTReMe Tracker