Leo nimefanikiwa kuipata 'bila ya shaka kwa ukamilifu wake' hotuba ya Mhe. J. M. Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipolihutubia bunge wakati wa kulifungua rasmi mjini Dodoma tarehe 30 Disemba, 2005. Baada ya shukrani ndefu kwa wale wote waliomsaidia 'kihalali na uovu' katika kufanikisha ushindi wa kishindo kwa Chama chake Mhe. Rais alianza moja kwa moja na tambo za ushindi wa kishindo wa CCM. Lakini pia alikiri uchanga wa demokrasia katika Tanzania kutokana na matokeo ya jumla ya uchaguzi. Ameelezea Majukumu ya Msingi ya Serikali ya Awamu ya Nne, na mwisho akatoa hadhari zake kwa viongozi wa serikali na wabunge, alisema "Mwishowe Tusialumiane".
Wananchi wote tuisome na kuielewa vizuri hotuba hiyo ili tuitumie kama 'reference' huko mbele ya safari.
Mwanzo wa Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya!