Mwanaharakati mwenzetu ametuaga kwa kusema kwamba hatokuwepo nasi kwa takriban mwezi mzima hivi! Duh! Kwa heri lakini sio mbaya hata siku moja moja ukishuka dimbani na kutupa salamu tu!
Haya ni majibu yangu ya chemsha bongo kuhusu Afrika ambayo nimeichomoa leo kutoka kwa Ndesanjo, sijagezea kaka!!. Hii ni changamoto kweli kweli juu ya uelewa wetu kuhusu bara letu Afrika kwani asilimia nilizozipata huko zinaonyesha ni kwa kiasi gani tunatakiwa kufanya jitihada za hali ya juu kuifahamu Afrika na kila kinachoihusu. Nimeifanya hata ile chemsha bongo ya kujaza ramani ya Afrika lakini nimeifanya kuanzia ile nyepesi kabisa mpaka ile ngumu kiasi, Duh!.
Ndesanjo amesisitiza tuweke picha kwenye blogu zetu, naweka hii hapa!
Hii ilikuwa mwaka 2004 katika Mkutano wa wadau wa uchaguzi kutoka katika makundi mbalimbali ya kijamii. Mimi 'niliyesimama' na Fredrick Mkatambo hapa kushoto kwangu tuliwakilisha kundi la watu wenye ulemavu kupitia Kituo cha Habari juu ya Ulemavu ICD. UNDP Dar es Salaam.
Mjadala kuhusu neno blogu kwa Kiswahili sijui umeishia wapi? Wakati huo huo nafanya jitihada za dhati kuipata hotuba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya kikwete alipolihutubia bunge jana.
Ingekuwa vizuri kama kiungo hiki ukakiweka katika blogu yako, ukitembelea kwenye blogu yangu utakuta nimekiweka upande wa kulia baada ya kitabu cha picha na nimekiita "Bunga bongo ya neno blogu kwa kiswahili.
Haya kazi kwako kaka.