DAMIJA MK MAKENE MICHUZI MWANDANI NDESANJO CHARAHANI AISHA ABDI MAVAZI SHAMIM MAGGID WATANZANIA Jumuia ya Wanablogu wa Tanzania
UNO AU EAC TANZANIA EU NASA REUTERS IPP Muungano wa Vijana Duniani dhini ya UKIMWI TIG IPP
NITUMIE BARUA PEPE

Hodi Hodi!!
Monday, December 26, 2005
Ni takriban miezi tisa sasa tangu nilipoanza kuperuzi blogu mbali mbali duniani. Kwanza iliniwia vigumu sana kuelewa maana halisi ya blogu, lakini kadiri siku zilivyozidi kusonga mbele bila kutusubiri akina sisi nilianza kwa taratibu kuelewa nini haswa lengo la blogu. Nimesoma blogu nyingi na kwa mra kadhaa kujaribu kutengeneza lakini kutokana na teknolojia hii kuwa ni mpya kabisa, iliniwia vigumu kwa kipindi chote hicho kuweza kutengeneza hiyo blogu yangu. Na hata zile ambazo nimejaribu kuzitengeza sikumbuki tena viunga vyake. Nilihamasika zaidi baada ya kuanzishwa kwa hizi blogu za Kiswahili, nakumbuka blogu ya kwanza kukutana nayo kwa lugha hii ni ya Kaka yangu Ndesanjo ambayo nilipitia moja makala zake zinazotoa maelekezo ya namna ya kunzisha blogu na kwa kiasi fulani nikafanaikiwa kuanzisha hii blogu yangu.

Madhumuni ya blogu hii ni kama kichwa chake kinavyosomeka "Mtandao wa Mawazo na Habari Chanya". Katika upashanaji habari kuna njia mbalimbali ambazo mpashaji na yule anayepashwa huzitumia. Habari yoyote ile inapotolewa, ni lazima itakuwa na lengo la kutolewa kwake. Kwa kipindi kirefu sana, Watanzania tumekuwa tukimezeshwa habari hasi zenye lengo la kutuondoa katika upekuzi na utafiti huku tukibaki na mapukupuku ya ujinga yatokanayo na utandawazi.

Tumetawaliwa kiakili kiasi kwamba tumesahau kabisa sisi ni akina nani. Sasa basi, kwa kupitia blogu hii, tutaamshana, kukumbushana na kupeana hamasa ya kujitambua kwa kupeana habari chanya na mawazo jengevu. Ili tuweze kujenga jamii chanya, tunahitaji umoja, mshikamano, kujielewa na kuelewana, kuhabarishana, n.k. Nipo nanyi nyote na ninaomba kujiunga nanyi.


NIMEPIGA HODI, BILA SHAKA NITAKARIBISHWA!!!!!!!! HONGERA WANABLOGU WOTE WA KISWAHILI!!
Muandishi: Kaka Poli Saa: 5:04 pm | Permalink |


14 Comments:


  • Saa: Monday, December 26, 2005 7:00:00 pm, Mtoa Maoni: Blogger Mija Shija Sayi

    Habari chanya + Jamii hasi = Jamii chanya.

    Karibu tupo.  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 2:51:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Ndesanjo Macha

    Karibu sana sana. Nimependa maelezo kuhusu lengo la blogu yako. Haya ndio maneno uliyosema:

    "Tumetawaliwa kiakili kiasi kwamba tumesahau kabisa sisi ni akina nani. Sasa basi, kwa kupitia blogu hii, tutaamshana, kukumbushana na kupeana hamasa ya kujitambua kwa kupeana habari chanya na mawazo jengevu."

    Kama lengo lako ni hili basi tuko pamoja. Kosa la kutojijua sisi ni nani hatuwezi kukubali liende kumaliza vizazi vijavyo. Karibu na ukaribishe na wengine. Uhuru!  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 2:53:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Ndesanjo Macha

    Ingawa mnajua kuwa hisabati zinanipiga chenga sana (ukiacha kuhesabu hela!) nimekubaliana na hesabu za Da Mija:
    habari chanya + jamii hasi= jamii chanya

    Nkya, una nyongeza hapo?  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 9:11:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Fikrathabiti

    Karibu brother katika uwanja wa mapambano ya kifikra kwani tumechoka kuishi katika Africa yetu kama si kwetu!

    Daima songa mbele na upingane na fikra potofu.Kwa vile huu ni mwanzo na tuko katika ardhi moja nitakua na deni la kukutafuta na tupate nafasi ya kuketi na kufanya tafakuri kina kuhusu mustakabali wa nchi yetu.

    Kwasasa niko Zanzibar la
    kini nitakutafuta pindi nifikapo Dar es salaam mwishoni mwa january.

    ALUTA CONTINUE!  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 9:12:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Fikrathabiti

    Karibu brother katika uwanja wa mapambano ya kifikra kwani tumechoka kuishi katika Africa yetu kama si kwetu!

    Daima songa mbele na upingane na fikra potofu.Kwa vile huu ni mwanzo na tuko katika ardhi moja nitakua na deni la kukutafuta na tupate nafasi ya kuketi na kufanya tafakuri kina kuhusu mustakabali wa nchi yetu.

    Kwasasa niko Zanzibar la
    kini nitakutafuta pindi nifikapo Dar es salaam mwishoni mwa january.

    ALUTA CONTINUE!  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 9:47:00 am, Mtoa Maoni: Blogger FOSEWERD Initiatives

    .......................Watanzania tumekuwa tukimezeshwa habari hasi zenye lengo la kutuondoa katika upekuzi na utafiti huku tukibaki na mapukupuku ya ujinga yatokanayo na utandawazi.................Ili tuweze kujenga jamii chanya, tunahitaji umoja, mshikamano, kujielewa na kuelewana, kuhabarishana>>>>>.........MAKOFI TAFADHALI KWA KAKA PORI!!

    mimi furaha yangu ni kubwa iliyoje kuona kuwa kila dakika mwanamapinduzi anazaliwa! karibu bloguni!!!! - inatia moyo kuona kuwa vijana sasa wanafikiria vizuri!! huwa ninashangaa hadi leo nikikuta vijana wana njaa tumboni lakini mawazo ni kwa ngono na utani! saa ya utani imekwisha! ISIWE NI LAANA KWETU KUZALIWA TANZANIA! TUNATAKA ULE WIMBO ANAOUPENDA SANA BEN UKIPIGWA -TANZANNIA TANZANIA, NAKUPENDA KWA MOYO WOTE- NA sisi tuwe tunaupenda tunauimba na kuuzimia pia!

    usishangae kuona watu wanaweza wasikuelewe unafanya nini...lakini jina lako litabaki katika kumbukumbu za taifa letu kwa maandishi ya dhahabu.....

    unachofanya kitatunusuru sisi na watoto wetu. kwa watoto wetu wasije kupata nuksi kufukua mikaburi yetu kisa kupima mafuvu kama tulikuwa na ubongo (John Msemo - mwanamaoni DHW)....kwetu sisi itanusuru maiti zetu zisipate bughudha kuamshwa amshwa na kuchinjwa na kupelekwa maabara-ipumuzike kwa amani!!!

    ninashangaa hadi leo ukisema jambo linalofanana na ukweli mfano, kukosoa sera au tatizo la utawala wale waheshimiwa wa ippmedia wanalichuja! wakati ni wao wenyewe waliomba maoni! nitatoa mfano, waliomba maoni pale paliandikwa upinzani umeanguka ...niliandika kuwa baba wa taifa alikuwa ni adui namba moja wa demokrasia! yeye aliwapeleka maafisa usalama wawe wapinzani, halafu akawaingilia kuwadhibiti wasifikirie uraisi, walipomzidi nguvu akawaita MBWA NA KURUDI JUKWAANI KUMPIGIA KAMPENI BEN!! - jamani huu si ukweli? kwani kuna siri hapa? wanawaogopa hata marehemu - kwa faida ya nani? BLOGU NI MWISHO WA MATATIZO MAONI YAKO HAKUNA ATAYECHUJA - NI UHURU KAMILI!

    hadi leo hii wapinzani wameonekana kuwa wahaini na mbwa mbele ya umma wa watanzania! nilisoma pale global voice kuwa kwa kipindi kifupi baada ya uchaguzi kandamizi wanablogu wa ethiopia waliongezeka hadi kufika zaidi ya milioni! nimeishakuwa ethiopia, mtadao bado ni chini na watu ni masikini kuliko sisi! hatutashindwa!!!

    pamoja na mengi - nia ni kupata makada wa kuzindua waliolala ili wachukue hatima zao mikononi mwao! wakati katika dunia ya sasa binadamu ndie huamua hatima yake dhidi ya mazingira na asili, kwa watanzania wengi ni usiku wa manane. akili zetu zimepata mafindofindo yanayowawezesha wengine kuamua hatma yetu!!. alika watu wengi kwenye mablogu na wewe tembelea ya wengine ili kuimarisha mtandao! karibu sana!!!  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 9:52:00 am, Mtoa Maoni: Blogger FOSEWERD Initiatives

    nilisahau,

    si ipp tu, ni vyombo vingi vya habari vimejaa unafiki na kuendeleza umasikini miongoni mwa watanzania! vinavyojitahidi ndio hivyo vinafungiwa fungiwa kidogo kidogo!

    nilisahau kusema kuwa globu la kiswahili nio muhimu ili lieleweke kwa wanajamii wa kawaida wa tanzania!

    na blugu lako si mchezo, maana lilikula utungu miezi 9!

    cheers  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 9:57:00 am, Mtoa Maoni: Blogger FOSEWERD Initiatives

    ushauri,

    kama unaweza hizo sentensi kali kali ulizoziweka hapo mwisho na kama zilivyonukuliwa kwa kutukuka na wanablogu wenzio, zingekaa mahali pa juu siku zote - labda baada ya kichwa cha blogu!! kwani ndio ufafanuzi wa ilani la blogu lako!  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 10:05:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Egidio Ndabagoye

    karibu sana tuantegeema mambo mengi ndani ya mtandao wa mawazo na habari chanya.
    Karibu  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 2:00:00 pm, Mtoa Maoni: Blogger mwandani

    karibu sana  
  • Saa: Tuesday, December 27, 2005 7:14:00 pm, Mtoa Maoni: Blogger boniphace

    Karibu mawazo chanya
    Karibu uje kuhenya
    Njua wataka onya
    Ujinga kufutilia.

    Nakukaribisha mwana
    Ulingoni kuchuana
    Hii ni mechi hiyana
    Wapaswa wazi kuhema.  
  • Saa: Wednesday, December 28, 2005 8:29:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Better tomorrow

    Karibu humu ndani..nasema heko kwa kujiunga na hili jahazi.Kumbuka kuweka mtazamo makini.Kheri kwa sikukuu ya kwanza.  
  • Saa: Tuesday, January 03, 2006 3:54:00 pm, Mtoa Maoni: Blogger Indya Nkya

    Karibu Ndugu yangu.  
  • Saa: Sunday, January 15, 2006 11:32:00 am, Mtoa Maoni: Blogger Reggy's

    ingawa nimechelewa kukuona, lazima ni muungwana kwa kukukaribisha, kwani ni wewe yule yule tunayetegemea kupata mawazo huru. KARIBU SANA  
eXTReMe Tracker