Baragumu wakaribishwa, Ila kwa taarifa yako, ni punde tu tumemuaga Msekwa. Huu ujio wako bila shaka umekuja kuongeza nguvu katika harakati zetu za kupanua wigo wa wanablogu mahiri, wenye dhamira ya kuiweka Afrika huru, Uhuru huo ni wa kujitambua sisi wenyewe kwanza, kutambua nyakati, na pia kutambua Mazingira. Ili kuweza kuyakabili hayo na mengine ni lazima tujue nini hasa kilitokea kisha kuuelewa kwa uzuri kabisa Kasri letu bado si pomoni hivyo ujio wako ni wa maana sana kwetu sisi 'washamba' tunaokumbatia utamaduni wetu. Karibu tukidumishe Kiswahili, tuutangaze utamaduni, na pia tulete mapinduzi kwa kusafisha kwanza fikra zetu halafu tuwaingie na wenzetu.
SAA YA UKOMBOZI NI SASA!!!!
Karibu Sana!!
Karibu hapa sisi tunaendelea na majadiliano bila kupigana, japo tunapingana. Endeleza kazi iliyoanzishwa na ndesanjo!
karibu sana Tutembelee sote tutafajirika kwa mawazo yako yaliyo chanya.